Tundu Lissu alivyowatekenya CCM

MWENYEKITI: Namwita Mheshimiwa Tundu Lissu na badala ya Mheshimiwa Mnyaa,
Mheshimiwa Amina Amour na Mheshimiwa Kafulila na Murtaza Magungu wajiandae.

MHE. TUNDU A. M. LISSU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kunipatia nafasi hii
kujadili hoja hii ya bajeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hiki ni kipindi kingine tena ambacho wengine wanakiita silly
season. Silly season, muda wa mambo ya kipuuzi, silly season.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kila mwaka, tunakutana katika Bunge hili kuzungumza na
kupitisha mambo ambayo tunajua hayatekelezeki. Serikali inakuja na bajeti, inakuja na ahadi
ambapo yenyewe inajua hazitekelezeki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wabunge wanasimama, wanasema wanaunga mkono mia kwa
mia, kinachofuata ni kuponda hicho walichokiunga mkono mia kwa mia kwa sababu wanajua
deep down ni uwongo, hakitekelezeki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, this is another silly season. This is another season to lie to
ourselves, to lie to our children, to lie to our country. We should be ashamed of ourselves. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana tulikuja tena kwenye silly season ya mwaka jana,
tukaambiwa na Serikali inayojua kwamba haya mambo hayatekelezeki, tukaletewa Mpango wa
Maendeleo wa Taifa wa miaka mitano. Serikali inayojua kwamba haya mambo hayatekelezeki,
ikatuambia kwamba kwa maneno yao, kwa maneno ya Mpango wenyewe, kuanzia sasa
tutatenga shilingi trilioni 8.6 ya mapato ya ndani kwa ajili ya Bajeti ya Maendeleo. Asilimia 35
Mpango wa Maendeleo wa miaka mitano, trilioni 43 approximately, tukaambiwa kwamba
tutatenga kila mwaka shilingi trilioni 8.6 ili kutekeleza mpango huu, another silly season. Tukaitwa St.
Gasper na Mheshimiwa Rais, tukalishwa, tukanyweshwa, tukapiga makofi, mwaka huohuo mwaka
jana, badala ya kutenga shilingi trilioni 8.6, wakatenga trilioni 4.9, silly season. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tukahoji hapa, tukahoji kwamba mbona mmesema mtatenga
shilingi trilioni 8.6, mbona mmetenga shilingi trilioni 4.9? Wakasema huu ni mwaka wa mpito. Sasa
leo, tunakutana hapa kujadiliana juu ya Mpango wa Maendelo na bajeti ambayo imetenga
shilingi trilioni 4.5 kwa ajili ya bajeti ya maendeleo, tuliambiwa, tutatenga kila mwaka shilingi trilioni
8.6, they knew they were lying, we knew they were lying; we should be ashamed of ourselves.
(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, we should be ashamed of this Government, we should be
ashamed of this party, and we should be ashamed of these Members of Parliament wanaopitisha
this kind of silly thing. (Makofi)


KUHUSU UTARATIBU
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, URATIBU NA BUNGE): Mheshimiwa
Mwenyekiti!
MWENYEKITI: Mheshimiwa Lissu naomba ukae. Mheshimiwa Lukuvi?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, URATIBU NA BUNGE): Mheshimiwa
Mwenyekiti, kuhusu utaratibu tu, namkumbusha uncle wangu, lugha hizi za kuudhi haziruhusiwi
humu Bungeni, tafadhali sana. Naomba tu aendelee na mchango wake, lakini lugha za kuudhi,
Kanuni zetu zinakataza, Kanuni ya 64.
MWENYEKITI: Mheshimiwa Lissu, ninaamini una hoja nyingi nzuri, unaweza kuwasilisha vizuri
na kila mmoja akaelewa, Kanuni ya 64 inatufunga kutumia maneno ya kuudhi wengine, naomba
uchangie hoja zako kwa uzuri, Serikali inakusikia, naomba uendelee.
MHE. TUNDU A. M. LISSU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Katika Mpango wa mwaka
jana tuliambiwa kwamba, Serikali itaziba mianya ya ukwepaji kodi, itapunguza misamaha ya kodi.
Hii lugha ni ya miaka mingi sana. Leo hii, mwezi huu, viongozi wetu wa kidini wa Baraza la
Maaskofu Tanzania wa Christian Council of Tanzania na wa BAKWATA, wametoa ripoti wanaiita
The One Billion Dolar Question; jinsi ambavyo Tanzania inapoteza fedha kutokana na mianya,
ukwepaji na misamaha ya kodi ambayo imepitishwa na Bunge hili na kila mwaka tunaambiwa
itashughulikiwa, lakini Serikali haifanyi hivyo, Wabunge wa Chama kinachotawala hawafanyi hivyo
na wao ndio wenye responsibility kwa sababu, wao ndio wengi. Kwa hiyo, this One Billion Dollar
Question, this One Billion Dollar Disaster ni disaster ya CCM and nobody else. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa wasiofahamu historia ya mambo haya, mwaka 1998,
Mheshimiwa Dkt. Abdallah Kigoda, alikuwa Waziri wa Madini, ndiye aliyeleta Muswada wa Sheria
ya Madini hapa. Mimi sikuwepo hapa, Mzee Cheyo, alikuwepo na kwenye Muswada, kwenye
mjadala wa kupitisha Sheria ya Madini ya Mwaka 1998, Hansard za wakati huo, Mheshimiwa Dkt.
Abdallah Kigoda na Mawaziri wenzake wakati huo waliliambia Bunge hili kwamba, sekta ya
madini italiingizia Taifa hili 52% ya revenue yote inayotokana na madini; we were told,
walituambia, walituahidi, leo hii viongozi wetu wa kidini wanatuambia katika mabilioni
yanayotokana na madini yetu, tunapata an average dola milioni 100 kama kodi na mirahaba na
vitu vinginevyo na wanasema kitu kingine kwamba, 65% ya hizo dola milioni 100 zinatokana na
kodi za wafanyakazi. Shame on this Government, shame on this party, shame on this people.
(Makofi)
MWENYEKITI: Samahani. Waheshimiwa ambao mnashabikia kwa kuongea, Kanuni
zinatuzuia. Huruhusiwi kuongea, isipokuwa kwa idhini ya Mwenyekiti au Spika. Muacheni achangie
vizuri, mtamshangilia huko nje.
Mheshimiwa Tundu Lissu, tafadhali!
MHE. TUNDU A. M. LISSU: Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tumekuwa na dini mpya Bunge hili
na kwa Serikali hii, tuna Miungu wapya na hawa Miungu wanaitwa wawekezaji. They are our new
Gods, they are untouchable; kila kitu ukifanya, eeh, wawekezaji, eeh, wawekezaji, don’t touch
them. Hawa ndio Miungu wetu wapya, what have they done for us out of other? No! Madini
wanatuambia, ni product inayoingiza more foreign exchange than any other. Hizo fedha
mlizotuambia zitakuja ziko wapi,? We have struck up and immerse riches off our cost. Natural gas,
kwa utaratibu wa hawahawa, wa chama hikihiki, wa Serikali hiihii, natural gas ambayo
imegunduliwa off our cost itakwenda njia ileile ya dhahabu na tanzanite. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mimi I have lost faith completely na Serikali hii. I have lost
faith na chama hiki. I have lost faith na watu hawa. Nawaomba Watanzania, watuunge mkono
katika hili. There is obsolutely no future kama nchi yetu itaendelea kuwa chini ya watu wenye
rekodi ya aina hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nimalizie maana wengine wanataka kuzungumza.
Mwalimu Nyerere kwenye kitabu chake cha ‘Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania’, alisema na
wala hatuwajibiki kuendelea na chama na Serikali hii na kama tukiendeleanayo, mbele ni giza
tupu, majuto ni mjukuu. Watanzania wenzangu hatuhitaji kuendelea na chama hiki, hatuendelei,
hatuhitaji kuendelea na this kind of silly na vitu ambavyo ni vya uongo, havitekelezeki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)
MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, hii sio kampeni.

No comments:

Post a Comment