Mkono 'kufilisi' nchi



KAMPUNIya mbunge wa Musoma Vijijini (CCM), Nimrod Mkono inadaiwa kulipwa na T anesco, takriban shilingi 18 bilioni kwa huduma ya ushauri, MAWIO imegundua.
Nyaraka ambazo gazeti hili limeona zinaonyesha kuwa tayari kampuni ya Mkono imetumia kiasi hicho kutoka shirika la umeme 'linalolegalega kifedha.
Mkono na kampuni yake ya Mkono & Co. Advocates ya jijini Oar es Salaam, amekuwa mshauri wa kisheria na wakili wa Tanesco tangu Mei 1995.
Nyaraka zinaonyesha kuwa shilingi 18 bilionj zimelipwa kwa ushauri na utetezi ambao kampuni ya Mkono imefanya katika minyukano ya kudaiana kati ya T anesco na kampuni 'nyingine ya umeme, Independent Power Tanzania Limited (IPTL).
Hivi sasa uhusiano wa Tanesco, kampuni ya umeme ya serikali na kampuni ya Mkono, umekuwa wa kilio kama mawasiliano ya ndani yanavyoonyesha.
barura ya Jenerali Robert Mboma, mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa Tanesco, ambaye inalalamikia ' maturnizi ya rnabilioni ya shilingi ya kampuni ya Mkono, tena bila mafanikio. Barua ya Mboma ya l0 Septemba 2013; kwenda kwa Mkono, inalalamikia matumizi ya kiasi hicho cha fedha katika mashauri ambayo yamechukua muda mrefu na bila kuleta tija. Barua yenye Kumb. Na. SEC.427/IPTU9/2013; ambayo imebeba kichwa cha maneno . kisemacho, "Ushauri ambao kampuni yako imetoa kwa Tanzania Electric Supply Company Limited," imenukuliwa kwa Waziri wa Nshati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo. "Kwa sasa, kulingana na kumbukumbu tuiizonazo, kampuni yako imekwishatumia takribani Sh. 18 bilioni kama gharama za ushauri katika kusimamia suala hili kufikia Aprili 2013," anaeleza Jenerali Mboma.
 Anasema, "Hiki ni kiasi kikubwa mno cha fedha za walipa kodi ambazo zingeweza kuwekezwa kwenye miradi mingine ya uzalishaji kwa manufaa ya Watanzania wote."
Kana kwamba hiyo haitoshi, Mboma anasema, "Tanesco inataka ieleweke kuwa inasikitishwa na namna kampuni yako ilivyotoa . ushauri wa kisheria kuhusiana na mivuteno iliyohusu Mkataba wa mauziano (PPA) wa tarehe 26 Mei 1995 kati yetu na IPTL, kwa vile ulivyotushauri na katika kuisimamia kesi tangu'ilipofunguliwa mwaka 1998."
Tanesco sasa inatuhumu kampuni ya mkono kutoishauri vizuri hadi kupoteza kesi yake dhidi ya IPTL. Kesi ambayo Tanesco inasema imeipoteza, kwa kutoshauriwa vizuri inahusu mkataba wa kununua umeme - Power Purchase Agreement (PPA) wa 26 Mei 1995.
Kampuni ya IPTL ndiyo kampuni ya kwanza ya nje kuingiza . mitambo ya kuzalisha umeme wa dharula nchini. Mitambo yake inatumia mafuta mazito (Industrial Oiezel Oil- 100); jambo ambalo linasababisha urnemeinadzalisha kuwa ghali kuliko ule wa kuzalisha kwa kutumia gesi na, au maji.
Taarifa kutoka ndani ya Tanesco zinasema, mbali na malipo Mkono, kampuni ya  IPTL hukomba kiasi cha  sh 1.8 bilion kila mwezi zikiwamalipo kwa gharama za kuweka mitambo yake nchini - Capacity Charge.
Mtoa taarifa kutoka ndani ya serikali anasema, kwa kuwa Tanesco inakabiliwa na ukata mkubwa wa fedha kutokana na mikataba ya kinyonyaji ya umeme, serikali hutoa kila mwezi, kiasi cha Sh. 3.8 bilioni kuwezesha shirika hila kununua mafuta ya kuendesha mitambo ya dharula .
Gazeti halikufanikiwa kumpata Jenerali Mboma. Mara zote simu yake ya mkononi ilijibu kuwa haipatikani.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi alisema hana taarifa ya suala hilo. Alitaka mwandishi amuonyeshe kwanza mawasiliano yaliyofanywa kati ya pande hizo mbili. Alipoelezwa gazeti limeona nyaraka hizo zilizonakiliwa kwa waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, Maswi alisema, " ... siwezi kulijua suala hilo." Naye Mkurugenzi Mtendaji Tanesco, Felchesmi Mramba, hakupatikana. Meneja Uhusiano wa T anesco, Badra Masoud alisema hawezi kuzungurnzia suala hila kwa kuwa ni jambo linalohusu Bodi.
 ilipokewa na mtu aliyejitambulisha ni dereva wake. Alisema basi wake yuko kwenye kikao.,Aliomba apigiwe baadaye.
Alipoitwa baadaye, dereva huyo alisema, “. .. bado yuko kwenye kikao, Alishauri atumiwe ujumbe ili . ampatie.
Gazeti lilituma ujumbe kwenye simu ya Mkono ambao ulisema, "Tunataka kujua msimamo wako kuhusu malalamiko ya T anesco kuwa kampuni yako ya uwakili imetumia 18 kwa kazi za ushauri na kusimamia kesi dhidi ya IPTL ... " Mkono hakujibu ujumbe huo. .
Kampuni ya Mkono imo katika umoja na kampuni ya SNR Denton. Imeelezwa kuwa umoja huo wa kampuni unaundwa na zaidi ya wanasheria 1,100 wa Uingereza, Marekani, Canada na Tanzania; na una makao makuu jijini London, uingereza.
Tanesco limeeleza kwamba lilishauriwa na wanasheria wa Mkono & Co. Advocates kuwa lina hoja za msingi kudai urekebishaji wa kiwango cha bei na kwamba "Tanesco watapaswa kudai kiasi kitakachokuwa kimezidi kutokana na ankara za IPTL zilizotozwa baada ya maamuzi.
" ... ulitushauri tutoe indhari ya madai ya ankara za ziada kwa IPTL. Tukapinga ankara za malipo zilizohusu gharama za kuweka mitambo - Capacity Charge. yote haya yalifanywa kwa kuzingafia ushauri wako," imeeleza barua ya Mboma kwa Mkono na kwamba hatua hiyo haikufanikiwa.
Katika barua , Tanesco inalalamikia kampuni ya Mkono kwamba pamoja na kutoa ushauri 30 Juni 2004 kuwa shirika hilo lina hoja za msingi na halali kuomba urekebishaji wa bei ya umeme na kurudishiwa malipo ya ziada, lakini 4 Oktoba 2012, Mkono alikwenda na mtizamo tofauti.
"Katika barua yako ya 4 Oktoba 2012, umesema kuna uwezekano mdogo sana wa kushinda kesi hiyo kutokana na kugundulika kwa baadhi ya nyaraka zilizodhoofisha utetezi uliotolewa mapema na shirika," barua ya Mboma inaeleza.
Inaongeza, "Ulitushauri kwa hoja nzito kuwa tupiganie usuluhishi na Benki ya Hong Kong - SCB HK au kampuni yako ielekezwe zaidi kuwasilisha ombi la kukataliwa kwa uamuzi unaoinufaisha benki hiyo,"Mboma anaeleza  mkono  kwa njia  ya malalamiko.
Barua ya shirika hila inajibu maelezo ya Mkono ya kutaka malipo ya zada ya fedha kwenye· kesi hiyo wakati Tanesco haioni manufaa ya malipo hayo.
Wakati wote wa mgogoro, fedha zilizokuwa zinabishaniwa mahakamani, ziliingizwa kwenye . akaunti maalum iliyofunguliwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
Kutokana na mfumo huo wa kubishania ankara, IPTL ilifungua malalamiko mbele ya Taasisi ya Usuluhishi wa Migogoro ya Uwekezaji (ICSID) wakitaka kupatikana tafsiri halisi ya eneo hila . kulingana na mkataba wa mauziano ya umeme.
Katika hatua hiyo, Tanesco inalalamikia kampuni ya Mkono ambayo iliiwakilisha mpaka pale shauri hila li!ipofutwa kwa manufaa ya IPTL kutokana na amri iliyotolewa 19 Agosti 2010. Kwa barua ya kampuni ya Mkono ya 4 Oktoba 2010, Tanesco inajulishwa kuhusu nia ya benki ya Standard Chartered Hong Kong (SCB HK) kufungua ombi la usuluhishi baada ya IPTL kuacha kuendelea kwa shauri. Matokeo yake, mbali ya kuihakikishia Tanesco kuwa itashinda, ikashauri pia shirika lielekeze kampuni hiyo ya uwakili kuendelea kutaka kusimamishwa kwa usajili wa malalamiko ya SCB Hlvrnbele ya ICSID kwa hoja kwamba SCB HK haina uhalali katika suala hilo. T anesco walitoa maelekezo hayo kwa ma~akili wa Mkono~', . Hata hivyo, T anesco inalalamika kuwa mawakili hao walishindwa kuzuia SCB HK kusajili malalamiko yake na hatimaye, "Ombi (letu) kuhusu suala hilo lilitupwa." "Usajili wa SCB HK ulikubaliwa na ICSIQ, na ukasikilizwa kama ulivyopangwa," imesema T anesco katika barua yake kwa kampuni ya Mkono.
Mara tu usikilizaji wa usuluhishi , ulipofungwa Aprili 2013, Tanesco inasema kampuni ya uwakili ya Mkono ilishauri shirika kufungua ombi la kucheleweshwa tamko la ICSID lakuipa SCB HK ushindi mpaka kwanza kusubiri uamuzi wa ombi la SCB HK lililokuwa likiendelea kusikilizwa kwenye  Mahakama Kuu ya Tanzania. "T anesco ilizuia, lakini pia; ilishindwa. ICSID ilisema kuwa itatoa tamko lake ndani ya miezi mitatu," barua ya Mboma inaeleza. Tanesco, mbali na kulipa mabilioni hayo ya shilingi kwa ushauri, imekuwa ikilipa fedha nyingi kwa makampuni yanayodai kutoa huduma za kisheria, ikiwamo kesi kati ya shirika hilo na makampuni ya Richmond Development Company (DRC), Dowans Holding na Dowans Tanzania Limited. Kuibuka kwa taarifa hizi kumekuja miaka sita baada ya Mkono kutajwa na kiongozi mkuu wa upinzani nchini, Dk. Willibrod Slaa kuwa ni miongoni mwa watuhumiwa 11 wa ufisadi nchini. Mbele ya umati mkubwa, kwenye mkutano wa hadhara katika Viwanja wa Mwembeyanga,' Temeke, Dar es Salaam,  Dk. Slaa . alisema Mkono, kupitia kampuni yake ya Mkono & Co. Advocates amekuwa akilipwa malipo makubwa, hasa yale yanayohusu kesi ya Valambhia, ambamo BoT inadaiwa jumla ya Sh. 60 bilioni. Ok. Slaa alisema, kwa mujibu wa Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG), kampuni ya Mkono tayari imelipwa zaidi ya Sh. 8.1 bilioni, fedha taslimu kwa kesi hiyo ambayo bado iko mahekamani Malioo havo wakati huo valikuwa sawa na asilimia 13.5 ya deni lote inalodaiwa BoT.
 Chini ya Kanuni za Malipo ya Mawakili na Uamuzi wa Gharama za Kesi za mwaka 1991 (T angazo la Serikali Na. 515la - I " 1995), ki':Vango cha malipo ya . mawakili katika kesi ambaao fedha : inayodaiwa ni zaidi ya Shs 18 milioni, kitakuwa asilimia tatu. Kwa kufuata masharfi ya sheria hii, kampuni ya Mkono ilipaswa kulipwa Sh. 1.8 bilioni. Aidha, kampuni ya Mkono inatajwa katika taarifa ya uchunguzi kuhusu tuhuma dhidi ya makampuni ya Tanfarms Ltd., Makinyumbi Estates Ltd., ' Centrepoint Investments Ltd., na Arusha Farms Ltd., yanayomilikiwa na V. G. Chavda kuhusiana na matumizi mabaya ya fedha za Debt Conversion Procramme. . '

No comments:

Post a Comment