Pamoja na list ya mambo lukuki ambayo wakuu mnamlaumu JK, lakini ni
kweli kuwa kuna kitu anafanya siyo kwamba amelele fofofo. Kuna mapungufu
pia ni kwa nia njema mnayaainisha kusaidia uboreshaji kazi.
Nimefuatilia na kuyaona baadhi ya mazuri ya JK Kama list inavyoainisha,
ninaweza kuwa na upungufu kidogo katika takwimu hii itatokana na mimi
kutumia kumbukumbu zangu nipo tayari kusahihishwa takwimu. Tupitie
mazuri ya JK HAPA CHINI
1. Mpango wa kuiruhusu bandari (THA) kufanya kazi kwa kuanza na
technologia mpya ili dereva tu ndiye awe anakwenda bandarini kupakia
mzigo na mengine yote yatamalizwa kwa njia ya mtandao, e-port. Kumbukeni
TICTS walikuwa na mkataba mbaya sana kwa miaka 15, na ulirejewa kwa
mazingira ya kutatanisha.
2. Dar tayari nyumba 50 zimeanza kutumia gesi kwa matumizi mbali mbali
ya ndani, kama ulaya na kwingineko kwa mara ya kwanza. Mikocheni
wameanza jiandaeni kuvuta gesi majumbani kwenu.
3. Magari yameaanza kutumia gesi japokuwa bado kuna baadhi ya vikwazo
kwa wasaidizi wa raisi. Mpango wa JK ilikuwa matuzi ya petroli katika
gari yapungue kwa 80%, lkn ukiritimba wetu umesababisha yapungue kwa 55%
4. Kivuko na daraja kigamboni.
5. Mradi wa daraja Maragalasi na lami Tabora – Itigi – Kigoma
6. Ujenzi wa barabara lami kutoka Mombo, Mtibwa turiani, Kilosa, Mikumi
na baadaye ifakara, mahenge, Malinyi, Songea. Pia Ifakara, Mlimba hadi
Njombe. Usafiri wa songea kupunguza safari kwa masaa 5.
7. Barabara ya Mafinga, Iringa, Kitonga, Ruaha Mbuyuni, Madaraja mawili
mpakani na morogoro imekwishapanuliwa kwa uboro wa hali ya juu. Kipande
cha Ipogolo kupandisha kwenda iringa mjini kimepanuliwa sana.
8. Bara bara ya Iringa Kwenda Dodoma Imekwishaanza
9. Bara bara ya Tunduma hadi Sumbawanga kuna makandarasi watatu wanashindana kwa ubora wa lami.
10. Viwanja vya ndege mikoani kuboreshwa.
11. Karekebisha mkataba wa Songas, ulikuwa hauruhusu mtu meingine yetote
awaye kujenga tena bomba la gesi. Sasahivi wakuu mnaruhusiwa kujenga
mabomba ya gesi kutoka Kusini.
12. Mkataba wa wachina na serikali kujenga bomba la gesi kutoka Mtwara hadi dar ili kuzalisha MG 2900 za umeme dar.
13. Barabara Dodoma, Manyara lami.
14. Ujenzi reli kutoka Tanga, Musoma, Uganda.
15. Ujenzi bandari, Tanga, Mtwara na Babamoyo
16. Uwanja wa Ndege Terminal two wajengwa.
17. Maeneo ya Umwagiliaji maji, hekari 20,000 zimejengwa na lengo ni ekari 1milioni.
18. Kilimo kwanza mashamba darasa na ongezeko la mavuno kwa ekari.
19. Tanzania ni ya kwanza kwa export afrika masharik na kati
20. Mradi wa makaa ya Mawe Mchuchuma na katewaka liganga kuzalisha MGW za kutosha nchi nzima
21. Mradi wa machimbo mgodi wa chuma Liganga, uzalishaji wa Titanium,
Vanadium, Fe kwa ajili ya utengenezaji nondo, malighafi ya mabati, vyuma
vya kujengea madaraja na maghorofa, kuweka pembezoni mwa mabarabara
kuzalishwa nchini. Viwanda vya kutengeneza vifaa vya ujenzi wa meli,
ndege, na magari kujengwa nchini.
22. Machimbo ya makaa yam awe Ngaka Mbinga Ruvuma, uwezo Kuzalisha pia umeme MG 400.
23. Hospitali upasuaji moyo kwa mara ya kwanza Tanzania.
24. Hospitali kubwa mingoni mwa zitakazoheshimika kujengwa Tanzania na Appollo ya India. Maradhi yote kutibiwa Tanzania.
25. Uboreshaji shirika la nyumba NHC, Baadhi ya watanzania kunufaika na
mikopo ya nyumba na nyumba kuanza kujengwa kwa spidi kali.
26. Ujenzi wa barabara nane Dar hadi chalinze.
27. Ufumuaji na ujenzi wa reli ya kati dar, hadi kigoma, mwanza, mpanda, Rwanda na Burundi.
28. Ubareshaji maabara shule za kata ($ 90Milioni)
29. Idadi ya walimu kwaajili ya shule za kata na nyinginezo kuanzia muda mfupi ujao, walimu elfu 40 kuhitimu kila mwaka.
30. Baadhi ya shule nyingi binafsi zimeanza kudorola au kufungwa
kabisha, wengi wamejiunga na shule za kata na ubora unapanda japo kwa
spidi ndogo.
31. Idadi kubwa ya wanafunzi vyuo vikuu, Udom uwezo elfu 40, SAUT elfu
15, UDSM Elfu 15, Ruco elf 2.5, Mkwawa elfu 2.5 Tumaini elfu 2, Open
University elfu 20 nk.
32. Wafanya biashara wamepewa kipau mbele term ya JK, Wengi husafiri na
Mheshimiwa Raisi kutafuta na kupata fursa za biashara nje.
33. Uhuru wa Vyombo vya habari, waandishi wanafanya mambo kwa uhuru
ambao wasingelithubutu enzi ya Mwalimu, Mwinyi wala Mkapa. Hata baadhi
ya ninyi wakuu, mnaruhusuwa kutoa mawazo yenu japo wengine wanatukana
matusi ya nguoni lakini JK anavumilia sana.
34. Amegundua fitna nyingi sana serikalini, majungu, uongo na sasa hivi
anakua mwangalifu sana katika maamuzi na inalazimika kuonekana kana
kwamba hana maamuzi ili awe na subira. (Ukiwa na hasiri usifanye
maamuzi, ahirisha upate busara)
35. Makampuni ya madini, yamekupali kuanza kulapa 30% kutoka faida zitakazo patikana kuanzia 2012.
36. Wapinzani wameanza kumwelewa na kumsifia kwa yale anayoyafanya vizuri.
37. Mnaweza ongeza list nyingine ili nije baadaye na listi ya faida za
kiuchumi kwa taarifa tu, inflation inachangiwa na gharama za chakula kwa
16%.
Kuna mambo madogo ya kiufundi yakirekebishwa inflation inapashwa iwe 8%
single digit. Mfano mahindi yanaoza Ruvuma, Iringa, na Sumbawanga
yangeweza kutoa mchango katika kupunguza gharama za chakula na mfumuko
wa bei ukashuka.Mengine mengi nitaongeza baadaye. Nadhani kwa faida ya
wakuu wangu, nitajitahidi kufuatilia pia ilani yake ili nilinganishe na
hayo hapo juu. Hata hivyo, ni ukweli kwamba kwa upanda wa barabara tu,
miaka 50 tangu uhuru lami ilifikia km 6000, JK Pekee ameweka mikataba ya
lami km 11,000.
Kuna vitu anafanya JK.
Mavi ni mavi tu hata ukiya pamba vipi bado yatabaki kuwa mavi.
ReplyDelete