Sheikh ponda apinga kauli ya mufti. Asema waislamu kutoshiriki sensa

Leo asubuhi sheikh ponda amepinga kauli ya mufti aliyoitoa jana akiagiza waislamu kushiriki ktk sensa ya mwezi agosti mwaka huu. akihojiwa na redio imaan iliyopo morogoro, sheikh ponda amesema kuwa bakwata ni moja ya taasisi za kiislamu hivyo mufti hawezi kuamua peke yake bila kuwashirikisha wajumbe kutoka taasisi nyingine.


"tulikutana dodoma na waziri wassira tukiwa wajumbe wa taasisi zaidi ya 10 za kiislamu, bakwata ikiwa moja wapo. msimao wetu ulikua mmoja kuwa hatutoshiriki sensa hadi yafanywe mambo mawili. la kwanza kipengele cha dini kiwekwe kwenye dodoso. la pili tume ya taifa ya sensa iwe na mchanganyiko wa wajumbe waislamu na wakristo. waislamu kwenye tume ni 20%." alisema ponda.


alipoulizwa nini kitaendelea akasema kuwa taasisi zote zinakutana leo na leo ama kesho watafanya press conference ili kuwaeleza watanzania maazimio yao. "Mufti amejidhalilisha. nina imani waislamu watafuata maelekezo yetu. mufti ataonekana jinsi asivyo fuatwa na kusikilizwa na waislamu wengi."


source: JF

No comments:

Post a Comment